Pages

Ads 468x60px

Featured Posts

Sunday, September 21, 2014

MBEYA CITY SERENGETI FIESTA HIYOOOOOOOO IMEWADIA NI TAR 28.09.2014



Wakazi wa Jiji La Mbeya Wakifuatilia Tamasha La Serengeti Fiesta Ndani Ya uwanja wa sokoine Hii ilikuwa ni mwaka jana 2013
 Haya tenaaaaa Wakazi wa Jiji la Mbeya Serengeti Fiesta Hiyoooooooo inanukia kwa sanaaaaaa……Ni tar 28.09.2014 ndani ya Jiji Lenye ukijani wa kutosha.Si yakukosa kabisa kwa wakazi woteee wa Mbeya City(Green City.Wasanii Kibaoo Kama…. Watakuwepo kupagawisha vya kutosha na bila kusahau kwenye jukwaaa kutakuwa na kila aina ya burudani na staili kalii kuliko.Usikoseeeeeeeeeeeeee Mana mwaka jana ilikuwa ni Shidaaaa sana pale sokoine Stadium  na mwaka huu tunasambaza upendooooo.Shuhudia picha ilivyokuwa mwaka jana
Nyomiiiii la Kutoshaaaa Wakifurahia Burudani Ndani ya uwanja wa Sokoine hii ilikuwa ni Mwaka jana  2013
BOFYA HAPA KUSOMA LIST YA WASANII WATAKAOPIGA SHOW MBEYA

Monday, August 11, 2014

KILI TOUR YAFUNIKA MBEYA


Mashabiki wakiingia katika uwanja wa New City Pub kushuhudia Kili Music Tour 2014.
Zembwela na Dulla wa EATV katika amsha amsha kabla ya show kuanza.
 Mkali kutoka Mbeya Izzo Bizness ndani ya backstage.
Chibwa anaefanya miondoko ya Ragga ndie aliifuungua show ya Kili Music Tour 2014 Mbeya
Shilole akionyesha uwezo wake wa kulishambulia jukwaa ikiwa ni pamoja na kumpandisha jukwaani mmoja wa mashabiki.
   Backstage: AY na DJ wake Arthur
 Rich Mavoko na madansa wake stejini
Mashabiki wakifurahia wasanii wanavyolishambulia jukwaa
 13,14. Massawe na Kimario kama wanavyopenda kuitwa waliendeleza utamaduni wao wa kufanya show kwa pamoja katika Kili Music Tour. 2014
 15. Wadau wakifuatilia kinachojiri jukwaani toka pembeni ya jukwaa la Kili Music Tour 2014
Mtoto wa nyumbani Izzo Bizness akiiwakilisha Mbeya katika Kili Music Tour 2014.
 Shangwe la kutosha kwa mtoto wa nyumbani
Profesa Jay akimbulisha Mbunge wa Mbeya Mjini Mheshimiwa Joseph Mbilinyi a.k.a Sugu.
DJ Mafuvu katika mashine akihakikisha wasanii na mashabiki wanakwenda sawa
  Zamu ya Weusi na Viburi kuifunga show ya Kili Music Tour, Mbeya
Profesa Jay na Sugu wakifuatilia michano ya Weusi
Mashabiki wakionyesha love ya kutosha kwa Weusi.

Friday, August 8, 2014

PICHA:::Wakali Kili Music Tour Wawasili Mbeya

Wasanii watakaopanda jukwaani katika tamasha la Kili Music Tour wamewasili jijini Mbeya. Wakali hao wanatarajiwa kufanya show katika viwanja vya New City hapo kesho wakiongozwa na msanii toka jijini hapo Izzo Bizness. Wengine waliowasili ni Profesa Jay, AY, MwanaFA, Joh Makini, Nikki wa Pili, Rich Mavoko, GNako Wara Wara na Chibwa huku Shilole akitarajiwa kuwasili hapo baadaye. 

 GNako na Rich Mavoko wakishuka kwenye ndege uwanja wa Songwe.

 DJ Mafuvu wa East Africa Radio/TV akiongozana na Profesa Jay



Friday, May 2, 2014

TASWIRA ZA BIRTHDAY YA MHE. JOSEPH MBILINYI aka SUGU.







Happy birthday baba Sasha wishing you many more & lots of blessings.
Images via Faiza Ally aka Mama Sasha

Tuesday, April 29, 2014

MAFUNZO YA KUPIGA ALA ZA MUZIKI KUANZA TENA MWEZI MEI‏

 Baadhi ya wanafunzi wakiwa kwenye mazoezi

Action Music Tanzania (AMTz) inatangaza fursa kwa watu wote kujiunga na mafunzo ya kupiga ala za muziki yanayoanza tarehe 3/5/2014, lengo likiwa ni kuwajengea uwezo wanamuziki wa kupiga ala na kufanya maonesho kwa weledi na utaalamu zaidi.
Baadhi ya wanafunzi wakiwa darasani

Mafunzo yanayotolewa ni pamoja na upigaji wa ala za muziki zikiwemo gita, kinanda, tarumbeta, saxophone, konga, drum set, na upigaji wa ngoma za asili. Pia yatatolewa mafunzo ya ‘body percussion’ yaani matumizi ya mwili katika kutengeneza midundo ya muziki.

Mafunzo hayo yanafanyika kwenye ofisi za AMTZ zilizopo maeneo ya Mwenge mtaa wa Umoja, nyuma ya magorofa ya jeshi na kwenye Idara ya Sanaa na Sanaa za Maonesho Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambapo ili kujiunga na mafunzo haya wasiliana nao kwa simu namba 0686928828/0653075791 ili kupata fomu za kujiunga na mafunzo.

Monday, April 21, 2014

SHINDANO LA TANZANIA MOVIE TALENTS MBEYA LAINGIA HATUA YA PILI LEO, KESHO WASHINDI KUPATIKANA



Kundi la Kwanza la Washiriki waliofanikiwa kuingia hatua ya pili ya Mchujo katika Mashindano ya Tanzania Movie Talents Mkoani Mbeya Wakipewa maelekezo kwaajili ya kuanza hatua ya mchujo leo.
 Washiriki wa Shindano la Tanzania Movie Talents Mkoani Mbeya kanda ya Nyanda za Juu Kusini wakiwa katika mazoezi mara baada ya kukabidhiwa Muswada (script) ikiwa ni hatua ya pili sasa ya shindano hili
 Ngoja tuangalie wenzetu wanafanyaje.....
 Wakitafakari muswada (script)..
Washiriki wakiendelea kuusoma Muswada (Script) kwa makini mara baada ya kukabidhiwa kwaajili ya hatua ya pili ya Shindano la Tanzania Movie Talents Mkoani Mbeya Kanda ya Nyanda za Juu Kusini.Picha zote na Josephat Lukaza wa Proin Promotions Limited - Mbeya

Na Josephat Lukaza wa Proin Promotions Limited - Mbeya

Leo Shindano la Tanzania Movie Talents limeingia ya hatua ya pili ya mchujo ambapo washiriki 30 wanatakiwa kupatikana kwaajili ya hatua ya tatu, washindi 30 watakaopatikana leo katika hatua hii ya pili wataendelea na hatua ya tatu ambapo washiriki 15 ndio watachukuliwa kwaajili ya kuendelea na mashindano hayo na hatimaye kupatikana washindi watatu bora ambao watawakilisha kanda ya nyanda za Juu Kusini na kwa kila mshindi mmoja kuibuka na kitita cha shilingi laki tano (500,000/=).

Mpaka sasa majaji wanaendelea kutafuta washiriki 30 watakaoendelea na shindano hilo kwa kanda ya nyanda za Juu Kusini na hatimaye kesho washindi watatu watapatikana na kuiwakilisha kanda ya kanda ya nyanda za Juu Kusini katika fainali kubwa itakayofanyika Mkoani Dar Es Salaam na hatimaye mshindi katika fainali hiyo kujinyakulia kitita cha Shilingi Milioni 50 za kitanzania (50,000,000/=)

Shindano la Tanzania Movie Talents linatarajiwa kumalizika kesho katika kanda ya nyanda za Juu Kusini Mkoani Mbeya na hatimaye kuhamia Kanda ya Kusini ambapo usaili utafanyika Mkoani Mtwara na wakazi wa Kanda ya Kusini wanaombwa kujitokeza kwa wingi ili kuweza kuonyesha vipaji vyao na kuweza kuitumia fursa hii, Vilevile fomu za usaili zitapatikana Siku hiyohiyo ya usaili na fomu hizo hazina gharama yoyote ile.

Sunday, April 20, 2014

MASHINDANO YA TANZANIA MOVIE TALENTS YAANZA MKOANI MBEYA

 Mshiriki wa Tanzania Movie Talents akihojiwa mara baada ya kumaliza usaili katika Shindano la Tanzania Movie Talents linaloendelea muda huu katika Ukumbi wa Benjamin Mkapa uliopo Soko Matola Mkoani Mbeya
 
Baadhi ya washiriki waliojitokeza kwaajili ya kuhudhuria usaili wa Shindano la Tanzania Movie Talents wakijadiliana jambo kabla ya kuanza kwa usaili.
 
 Washiriki waliojitokeza kwaajili ya kushiriki mashindano yya Tanzania Movie Talents wakijaza fomu kwaajili ya usaili wa shindano la Tanzania Movie Talents linaloendelea Mkoani Mbeya ikiwa unawakilisha Kanda ya Nyanda za Juu Kusini
 Baadhi ya washiriki kutoka Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Mkoani Mbeya wakisubiri shindano la Tanzania Movie Talents kuanza.
Kundi la Kwanza La vijana waliojitokeza kwaajili ya usaili wa Shindano la Tanzania Movie Talents linaloendelea mkoani Mbeya muda huu.Picha na Josephat Lukaza wa Proin Promotions Limited - Mbeya
Hatimaye Shindano la Tanzania Movie Talents limeanza rasmi leo katika Kanda ya Nyanda za Juu Kusini ambapo usaili huo unafanyika Mkoani Mbeya Katika Ukumbi wa Benjamini Mkapa uliopo Soko Matola Mkoani Mbeya.

Mpaka sasa Washiriki wapatao 150 wamejitokeza kwaajili ya kushiriki shindano hili la Tanzania Movie Talents ambapo washindi watatu kutoka kanda ya Nyanda za Juu Kusini watazawadiwa kitita cha Shilingi laki tano za Kitanzania na Baadae kupewa Tiketi ya Kuelekea Mkoani Dar Es Salaam kwaajili ya kushiriki fainali itakayowakutanisha Washindi waliopatikana katika Kanda ya Ziwa, Kati na kanda zilizobakia za Pwani na Kaskazini na mshindi katika fainali hiyo atajinyakulia Kitita Cha Shilingi Milioni 50 za kitanzania pamoja na Mikataba minono kutoka Kampuni ya Proin Promotions Limited na washindi kumi katika fainali hizo watakuwa chini ya kampuni ya Proin Promotions Limited na kuweza kutengeneza filamu ya Pamoja ambapo watanufaika na Mauzo ya filamu yao.
Mashindano ya Tanzania Movie Talents yataendelea Mkoani Mbeya kwa Siku nne ambapo siku ya jumanne washindi wa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini watapatikana na kupewa Zawadi zao.